Jua Haki Zako

Kenya: Wakulima wadogowadogo washinda kesi ya Sheria ya Mbegu na Mimea dhidi ya KEPHIS

Informações:

Synopsis

Nchini Kenya, Sheria ya Mbegu na Mimea (The Kenya Seed and Plants Varieties Act), ambayo ilitishia kuwatoza faini na kuwafunga jela wakulima wadogo kwa kugawana mbegu ambazo hazijaidhinishwa, iliamuliwa kuwa kinyume cha katiba. Mahakama ya Kikatiba katika kaunti ya Machakos nchini Kenya ilitoa uamuzi wa kihistoria Novemba 27 2025 kuhusu uhalali wa Sheria ya Mbegu na Aina za Mimea. George Ajowi amekuwa akifuatilia kesi hii na kuandaa taarifa ifuatayo.